Kwa mujibu wa shirika la habari ABNA kwa kunukuu Al Jazeera, Qatar, Misri na Uturuki kwa kutoa taarifa ya pamoja walitangaza: "Sisi kama nchi za wapatanishi, tunalaani ukiukaji wa mara kwa mara wa mapatano ya kusitisha vita na Israel katika Ukanda wa Gaza na tunaitaka jamii ya kimataifa kuishinikiza Israel kuzingatia makubaliano ya kusitisha vita."
Katika taarifa ya pamoja ya Qatar, Misri na Uturuki kuhusu hili imeelezwa: "Tunataka ulinzi wa raia, vituo vya matibabu na wahudumu wa misaada, pamoja na kupelekwa kwa misaada Gaza. Vitendo vya ukiukaji vya Israel vinatishia mchakato wa kupunguza mvutano na vinazidisha mateso ya raia katika Ukanda wa Gaza. Vitendo vya ukiukaji vya Israel vitadhoofisha utekelezaji wa awamu ya pili, hasa baada ya Hamas na makundi ya Kipalestina kukubaliana na ramani ya njia."
Maoni yako